Shule za Msingi mkoani Dar es Salaam:Msongamano wa wanafunzi bila vitabu vya kiada vya kutosha
Uwazi iliyopo Twaweza imetoa muhtasari wa sera kuhusu mazingira ya kusomea kwenye shule za msingi za Serikali za Dar es Salaam. Kwenye muhtasari huu inaripotiwa kuwa pamoja na kuwa karibu na mahali sera zinapotungwa, shule za Dar es Salaam zina mahitaji makubwa ya vyumba vya madarasa na vitabu vya kiada.
Muhtasari huo unaitwa, “Shule za Msingi mkoani Dar es Salaam:Msongamano wa wanafunzi bila vitabu vya kiada vya kutosha.” unaonesha kuwa kwa wastani wanafunzi 81 wanakaa ndani ya darasa ambalo linatarajiwa kuwa na wanafunzi 40. Muhtasari huu unadokeza kuwa karibu nusu ya shule zilizotembelewa wanafunzi wanalazimika kukaa sakafuni kwa kuwa hakuna madawati ya kutosha. Uchambuzi huu umejenjwa kwenye utafiti kwenye sampuli ya shule 40 za msingi za Ilala, Temeke na Kinondoni, na ulifanyika kati ya Agosti na Desemba mwaka 2010. Soma muhtasari mzima.
Endelea kusoma: Elimu Tanzania Elimu ya Msingi machapisho Twaweza.Uwazi
unaweza pia kupenda...
- Shule za msingi za Serikali Dar es Salaam:Vyoo vibovu, michezo kidogo. (2 Jun 2011)
- Matokeo yakipuuzwa, ukaguzi wa nini? (24 May 2011)
- Wabunge waongeaji Bungeni ndio hutetea viti vyao tena? (14 Apr 2011)
- Je Watoto Wetu Wanajifunza? Kuhesabu na Kusoma Katika Afrika Mashariki (28 Jul 2011)
- Shule za Sekondari Tanzania: Wanafunzi wengi, fedha kidogo (28 Oct 2010)
- Ruzuku ya wanafunzi kwa ajili ya Elimu: Ni lini italeta mabadiliko? (28 Oct 2010)
- Dar es Salaam wanachukuliaje utawala? (19 Dec 2012)

