Twaweza.org

Wananachi watakiwa kufuatilia pesa za shule za sekondari

Twaweza Tanzania inashirikiana na shirika la utetezi wa elimu, HakiElimu na Policy Forum kufuatilia utekelezaji wa ahadi ya serikali kupeleka pesa za uboreshaji wa elimu ya sekondari kila shule ya serikali nchini. Ufuatiliaji huo uliozinduliwa jana umeanza baada ya serikali kuahidi kuwa ifikapo Januari 31, 2011 asilimia 40 yaani shilling 10,000 ya fungu la mwaka mzima kwa kila mwanafunzi itakuwa imefika mashuleni tayari. Jumla ya ruzuku ya uboreshaji elimu kwa kila mwanafunzi kwa mwaka ni shilingi 25,000.

Meneja wa Programu wa Twaweza Tanzania, aliyekuwapo katika uzinduzi, Joseph Ngwegwe, amewataka wazazi, jamii kwa ujumla na waalimu kufuatilia mashuleni kujua iwapo pesa zimefika na kutoa taarifa kwa namba maalumu. “Wazazi wanatakiwa kuuliza mashuleni iwapo pesa zimefika, sababu juhudi zao zitasaidia watoto wao kufanya vema katika mitihani, na kupata ujuzi,” alisema.  Kusoma taarifa zaidi kuhusu ufuatiliaji huu soma hapa chini

Majira

Mtanzania

Mwananchi

Nipashe

The Citizen (Kiingereza)

Endelea kusoma: Hakielimu policy forum SEDP II Twaweza

unaweza pia kupenda...

 

Tafsiri