<?xml version="1.0" encoding="iso-8859-1" ?>
<rss version="2.0" xmlns:media="http://search.yahoo.com/mrss/" xmlns:dc="http://purl.org/dc/elements/1.1/" xmlns:geo="http://www.w3.org/2003/01/geo/wgs84_pos#" xmlns:georss="http://www.georss.org/georss">
<channel>
<title>Matangazo :: Vyombo vya habari :: Twaweza.org</title>
<link>http://twaweza.org</link>
<description>Twaweza.org can make it happen.</description>
<language>sw-sw</language>
<image>
<url>http://twaweza.org/images/twaweza-logo.jpg</url>
<title>Matangazo :: Vyombo vya habari :: Twaweza.org</title>
<link>http://twaweza.org</link>
</image>
				<item>
					<title><![CDATA[Wananchi Wazungumza kuhusu Matokeo ya Kidato cha Nne]]></title>
						<link>http://twaweza.org/index.php?i=1038</link>
						<guid isPermaLink="true">http://twaweza.org/index.php?i=1038</guid>
		
							<description><![CDATA[<p>
	Wazazi wana ufahamu kuhusu mwendelezo wa kuanguka kwa ubora wa elimu ya sekondari, na kwa kiasi kikubwa wanatupa lawama kwa serikali na walimu kwa kuanguka huko. Wazazi wanaitaka serikali kuongeza idadi ya walimu waliofuzu na wenye sifa stahiki na wanaolipwa vizuri iliwasaidie kuboresha elimu nchini Tanzania.</p>
<p>
	Matokeo haya yamechapishwa katika muhtasari wa Twaweza unaoitwa Matokeo ya Mtihani wa Kidato<br />
	cha Nne: Wananchi wazungumzia mgogoro wa kujifunza Tanzania. Muhtasari huo umeandaliwa kutokana na takwimu zilizokusanywa kupitia utafiti wa Sauti za Wananchi, ambao ni utafiti wa njia ya simu za mkononi wenye sura ya uwakilishi wa kaya kitaifa kote Tanzania Bara. Wahojiwa waliombwa kueleza maoni yao kuhusu elimu, na kubaini changamoto na njia za kuongeza ubora. Takwimu zilizotumika kwenye Muhtasari huu zilikusanywa kati ya tarehe 18 Machi hadi 3 Aprili, 2013 kabla ya tangazo la serikali la kurekebisha matokeo ya Kidato Cha Nne ya mwaka 2012.</p>
<p>
	Miongoni mwa waliohojiwa, asilimia 68 ya wananchi walikuwa na taarifa kwamba matokeo ya Mitihani ya Kidato cha Nne ya 2012 yalikuwa yamechapishwa. Idadi kubwa ya wahojiwa walionesha kutambua kuanguka kwa ubora wa elimu ya sekondari katika miaka kumi iliyopita, ambapo wananchi asilimia 83 walionesha kwamba elimu ilikuwa imeporomoka. Idadi hiyo inaendana na takwimu rasmi zikiwamo zile za Wizara ya Elimu zinazojulikana kama Basic Education Statistics in Tanzania (BEST).</p>
]]></description>
							<pubDate>Tue, 14 May 2013 05:54:00 +0000</pubDate>
				
				</item>
	
				<item>
					<title><![CDATA[Sauti za Wananchi]]></title>
						<link>http://twaweza.org/index.php?i=1012</link>
						<guid isPermaLink="true">http://twaweza.org/index.php?i=1012</guid>
		
							<description><![CDATA[]]></description>
							<pubDate>Thu, 14 Feb 2013 04:19:00 +0000</pubDate>
				
				</item>
	
				<item>
					<title><![CDATA[Mpango wa KiuFunza - Kiu ya Kujifunza - Wazinduliwa]]></title>
						<link>http://twaweza.org/index.php?i=1007</link>
						<guid isPermaLink="true">http://twaweza.org/index.php?i=1007</guid>
		
							<description><![CDATA[<p><br>
	Mpango mpya wa utekelezaji wa sera za Elimu, inayojulikana kama KiuFunza, itakayojaribu kutekeleza utaratibu wa kupeleka kiasi kamili cha ruzuku kwa kila mwanafunzi moja kwa moja shuleni kwa ajili ya uendeshaji wa shule; na kuwalipa walimu motisha kwa ufundishaji makini umezinduliwa. Mpango wa KiuFunza unalenga kutafuta njia bora zaidi za kuinua matokeo ya ujifunzaji kwa wanafunzi katika shule za msingi.</p><br>
<p><br>
	Mpango huu utatekelezwa katika Halmashauri 11 zilizochaguliwa kinasibu katika kipindi cha 2013 na 2014. Katika kila Halmashauri shule 35 zitashiriki. Wilaya zitakazohusika katika mpango huu ni: Karagwe, Kigoma Vijijini, Geita, Kahama, Kondoa, Korogwe Vijijini, Lushoto, Sumbawanga Vijijini, Mbozi, Mbinga na Kinondoni.</p><br>
<p><br>
	KiuFunza ni jitihada inayotekelezwa kwa ushirikiano baina ya Twaweza, <a href="http://www.costech.or.tz/">Tume ya Sayansi na Teknolojia (COSTECH)</a>, na watafiti wa kimataifa kutoka <a href="http://www.povertyactionlab.org/">Abdul Latif Jameel Poverty Action Lab (J-PAL)</a> ya <a href="http://www.mit.edu/">Massachusetts Institute of Technology (MIT)</a>. Lengo la mpango huu ni kupata ushahidi wa kuaminika kisayansi, kupitia utafiti makini, kuhusu mbinu ambazo zina ufanisi wa uhakika katika kuwasaidia wanafunzi kujifunza. Mpango huu utajaribu kutekeleza njia mbadala ya kutekeleza sera ya sasa ya kupeleka ruzuku ya uendeshaji shuleni, na pia utatekeleza mbinu mpya ya kuwalipa walimu motisha ya fedha kwa ufundishaji makini utakaofanya matokeo ya kujifunza kwa wanafunzi kuwa bora kuliko ilivyo sasa.</p><br>
<p><br>
	Mpango huu wa utafiti ulizinduliwa katika semina ya Wadau iliyofanyika katika Ukumbi wa Makumbusho ya Taifa tarehe 23 Januari, 2013. Mgeni rasmi katika semina hiyo alikuwa Mh. Hawa Ghasia (MB), Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa. Watoa mada walitoka Tume ya Sayansi na Teknolojia (COSTECH), Chama cha Walimu Tanzania (CWT), waheshimiwa wabunge, na Twaweza. Mikoa na halmashauri zitakazoshiriki katika utekelezaji wa mpango huu pia ziliwakilishwa na Makatibu Tawala, Wakurugenzi wa Halmashauri, Wenyeviti wa Halmashauri na Maafisa Elimu. Wabunge pia walishiriki.&nbsp;</p><br>
<p><br>
	<a href="http://twaweza.org/go/education-rct-launch">Endelea kusoma (Kiingereza)</a></p><br>
]]></description>
							<pubDate>Sat, 02 Feb 2013 10:14:00 +0000</pubDate>
				
				</item>
	
				<item>
					<title><![CDATA[Toa maoni, jishindie kompyuta]]></title>
						<link>http://twaweza.org/index.php?i=989</link>
						<guid isPermaLink="true">http://twaweza.org/index.php?i=989</guid>
		
							<description><![CDATA[<p>
	Ndugu msomaji, hivi karibuni Serikali ya Tanzania imeahidi kuboresha&nbsp;utoaji wa huduma kwa wananchi.<br />
	Kupitia mpango huu, Serikali inataka kukusikia.</p>
<p>
	Toa maoni yako kuhusiana na upatikanaji wa huduma za msingi za&nbsp;kijamii; maji, elimu na afya.</p>
<p>
	<strong>Tuambie wazo moja kuboresha elimu, afya au maji. Halafu,&nbsp;tuambie mwananchi afanye nini kuleta mabadiliko.</strong></p>
<p>
	Kila baada ya miezi mitatu kwa mwaka 2013, maoni kumi bora&nbsp;yatachaguliwa na kompyuta ndogo (laptops) zitatolewa&nbsp;kwa washindi na kwa shule watakazozichagua.&nbsp;Pia, maoni ya washindi yatachapishwa kwenye&nbsp;vitabu na tovuti.</p>
<p>
	<strong>Tuma maoni yako kabla ya tarehe 1 Novemba, 2013</strong></p>
<p>
	<strong>Anuani: </strong>OGP Tanzania, S.L.P 38342, Dar es Salaam<br />
	<strong>Barua pepe: </strong><a href="mailto:unasemaje@gmail.com">unasemaje@gmail.com</a></p>
<p>
	<strong>Kumbuka kuweka taarifa hizi:</strong><br />
	Tarehe<br />
	Majina kamili, umri wako, jina la shule; jinsia (me/ke)<br />
	Anuani kamili: SLP na makazi (kata, wilaya na mkoa); namba ya&nbsp;simu; barua pepe</p>
]]></description>
							<pubDate>Fri, 14 Dec 2012 07:03:00 +0000</pubDate>
				
				</item>
	
				<item>
					<title><![CDATA[Serikali inakusanya maoni ya wananchi kuhusu huduma za afya, elimu na maji ]]></title>
						<link>http://twaweza.org/index.php?i=985</link>
						<guid isPermaLink="true">http://twaweza.org/index.php?i=985</guid>
		
							<description><![CDATA[<p><br>
	Kama sehemu ya mchango wake katika Mpango wa Kimataifa wa Kuendesha Shughuli za Serikali kwa Uwazi (OGP), Twaweza imezindua shindano litakalohusisha utoaji wa kompyuta ndogo (laptops) kwa washindi na kwa shule watakazozichagua. Washindi watakuwa wale watakaotoa maoni bora zaidi kuhusu namna huduma za afya, elimu na maji zinavyoweza kuboreshwa na mwananchi anapaswa kufanya nini kuleta mabadiliko.</p><br>
<p><br>
	Serikali ya Tanzania inakusanya maoni ya wananchi kuhusu namna ya kuongeza ubora, uwazi na uwajibikaji katika utoaji wa huduma hizo. Twaweza inasaidiana na Serikali katika jukumu hili, kwa kutumia njia ya utayarishaji machapisho-pendwa na kusaidia kupitia maoni hayo.</p><br>
<p><br>
	Kati ya machapisho-pendwa yatakayotumika kuhamashisha shindano hili, ni vijitabu vya vibonzo vilivyoandaliwa kwa kushirikiana na <a href="http://tamashavijana.com/">Tamasha</a>. Maelezo yake yanapatikana katika sehemu ya <a href="http://twaweza.org/go/youth-booklets">Sherehekea mawazo yako</a></p><br>
<p><br>
	Rakesh Rajani, Kiongozi wa Twaweza, alisema: <em>&ldquo;Mpango wa Kimataifa wa Kuendesha Shuguli za Serikali kwa wazi&nbsp; ni mkabala mpya wa utawala unaozingatia ubia kati ya wale wanaotawala na wale wanaotawaliwa ili kutafuta ufumbuzi kwa changamoto kubwa zaidi zinazotukabili. Kukusanya maoni ya raia kuhusu namna ya kuongeza ubora katika utoaji huduma ni hatua muhimu ya kwanza katika kuhakikisha kwamba dira hii inakuwa kweli na Twaweza inafurahi kuweza kusaidiana Serikali kwa kufanya wito huu kwa watu usambae zaidi ili kukusanya maoni.&rdquo; &nbsp;</em></p><br>
<p><br>
	Shindano hili limezinduliwa kwa tukio maalum lililohudhuriwa na Kiongozi wa OGP Tanzania Mheshimiwa Mathias Chikawe (<a href="http://www.sheria.go.tz/">Waziri wa Katiba na Sheria</a>), Richard Mabala (<a href="http://tamashavijana.com/">Mkurugenzi, Tamasha</a>) na John Ulanga (<a href="http://www.thefoundation.or.tz/?lang=2">Mkurugenzi Mtendaji, Foundation for Civil Society</a>).</p><br>
]]></description>
							<pubDate>Wed, 12 Dec 2012 13:24:00 +0000</pubDate>
				
				</item>
	
				<item>
					<title><![CDATA[Change ni mimi. Ni wewe. Ni sisi]]></title>
						<link>http://twaweza.org/index.php?i=979</link>
						<guid isPermaLink="true">http://twaweza.org/index.php?i=979</guid>
		
							<description><![CDATA[<p><br>
	<em>&ldquo;Fikra husafiri, tunaona jinsi wenzetu wanavyoishi na kujiletea mabadiliko, tunajiuliza &lsquo;kama wao wanaweza, kwa nini sisi tusiweze?&rsquo;, tunapata cha kujifunza, tunapata maana, tunatengeneza zana, tunajipanga, tunachukua hatua.&rdquo;</em></p><br>
<p><br>
	&lsquo;Ni Sisi&rsquo; ni kampeni mpya inayohamasisha fikra kwamba wananchi wanaweza kujiletea mabadiliko wenyewe, badala ya kusubiri serikali, wanasiasa, wafadhili au AZISE kuwafanyia kila kitu.</p><br>
<p><br>
	Taasisi ya Twaweza inaamini kwamba kwa kuamua na kuchukua hatua, wananchi kote Afrika ya Mashariki wanaweza kuleta mabadiliko makubwa ya kudumu na kuweka msukumo kwa ajili ya maendeleo yao wenyewe.</p><br>
<p><br>
	Kauli mbiu hiyo ya kempeni iliyo katika lugha ya Ki-Swahili inaweza kufasiriwa kama &lsquo;Mabadiliko ni mimi. Ni wewe. Ni sisi.&rsquo; Lengo ni kutoa msukumo kwenye midahalo na kuchukua hatua katika dhana hii ya &lsquo;Ni sisi&rsquo;, kuhusu namna gani tunaweza kutoa mchango kwa jamii, maendeleo na maisha yetu. Yanayozungumzwa kwenye kampeni hiyo yanatokana na hali halisi ya maisha ya watu na kumpa changamoto kila mwananchi ili afikiri kuhusu masuala haya na kujitafutia suluhu kwa matatizo wanayokabiliana nayo.</p><br>
<p><br>
	Kampeni itahusisha shughuli mbalimbali nchini Tanzania, Kenya na Uganda. Kazi kuu ni matangazo sita ya televisheni kuhusu utumishi wa umma (PSAs). Kila tangazo la umma litamwonyesha mtu mmoja jasiri anayechukua hatua madhubuti au ile isiyo ya kawaida ili kulikabili tatizo fulani na, kwa kufanya hivyo, anawatia hamasa wengine kujiunga naye. Kisha kwa pamoja wanaleta mabadiliko katika jamii yao.</p><br>
<p><br>
	Kampeni hiyo pia itahusisha vipindi vya redio, machapisho, masuala yasiyozoeleka sana na yale yanayotazama mbali zaidi ya taratibu za kawaida. Twaweza inashirikiana na washirika kadhaa ili kutayarisha vipindi vya majadiliano, katuni, video za muziki na maonyesho ya barabarani, sambamba na matangazo ya utumishi wa umma kupitia majukwaa haya mbalimbali. Shughuli zote hizi zinalenga kusukuma wazo kuu la mabadiliko yanayoletwa na wananchi wenyewe.</p><br>
<p><br>
	Kiini cha ujumbe wa kampeni ni kuonyesha jinsi gani sote katika jamii tunavyohusiana &ndash; kile kinachotuunganisha.Kwa upande mmoja, tunaweza kujichukulia kwamba sisi ni tofauti na serikali na watendaji wa umma, au tunaweza kujiona kama washiriki kwenye uwajibikaji ili kufanikisha ufanisi mzuri katika utendaji. Tunaweza kusubiri siku nzima ili mtu mwingine afanye kazi kwa ajili yetu, au tunaweza kuwa sehemu ya kundi linalotafuta suluhu. Tunaweza kuwa watu wa kulalamika tu bila mwisho, au tunaweza kuchukua hatua na sisi wenyewe kuleta mabadiliko na kuwawajibisha wale wenye wajibu. Ulimwengu tunamoishi ni ule ambao tumesaidia kuumba uwe vile ulivyo au kuufanya utokee ulivyo; na ni sisi ndiyo tunaoweza kuufanya ulimwengu uwe mahali bora zaidi.</p><br>
<p><br>
	<a href="http://www.flickr.com/photos/twaweza/sets/72157632007310638/">Flikr</a></p><br>
<p><br>
	<a href="http://www.youtube.com/user/Twaweza">You Tube: </a><a href="http://youtu.be/Mkog1kftwds">Daladala</a></p><br>
]]></description>
							<pubDate>Wed, 14 Nov 2012 13:19:00 +0000</pubDate>
				
				</item>
	
				<item>
					<title><![CDATA[Mkutano wa Uwazi-Afrika Unalenga Kuleta Demokrasia kwenye Masuala ya Data]]></title>
						<link>http://twaweza.org/index.php?i=977</link>
						<guid isPermaLink="true">http://twaweza.org/index.php?i=977</guid>
		
							<description><![CDATA[<p><br>
	Mkutano wa Uwazi-Afrika ulifanyika Zanzibar kuanzia tarehe 7 hadi 8 Oktoba, 2012. Mkutano huo ulijikita kwenye uwazi wa data barani Afrika mada mbalimbali ziliwasilishwa na baadhi ya wanazuoni&nbsp; muhimu katika uwanja huo wa data, miongoni mwao walikuwa Amadou Mahtar Ba wa <a href="http://www.africanmediainitiative.org/">Africa Media Initiative</a>, Jay Bhalla wa the Open Institute na Alex Howard wa <a href="http://oreilly.com/">O&rsquo;Reilly Media</a>. Mkutano ulifunguliwa na Naibu Waziri wa Sheria na Mambo ya Katiba Angela Kairuki aliyetoa mada kuhusu uongozi wa serikali katika ushirikiano na Serikali Uwazi (<a href="http://www.opengovpartnership.org/">Open Government Partnership</a>) na vilevile hotuba kuu ya ufunguzi ilitolewa na January Makamba, Naibu Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia.</p><br>
<p><br>
	Rakesh Rajani wa Twaweza alizungumza katika mkutano huo kuhusu ubunifu unaowagusa watu (Human Centred Design), na aliwapatia washiriki miongozo muhimu ya kuunda na kutekeleza kwa mafanikio miradi ya kiteknolojia yenye kuleta tija kwa watu. Akitolea&nbsp; mifano ya miradi miwili iliyoshindwa iliyofadhiliwa na Twaweza -- <a href="http://www.huduma.or.ke/">Huduma</a> na <a href="http://www.daraja.org/">Daraja</a> &ndash;Rajani alisisitiza mchakato wa usanifu unaoanza na watumiaji pamoja na wengine wanashikishwa kwenye hatua za mchakato&nbsp; na kisha kufanya kazi kurudi nyuma hadi kufikia mafanikio. Vile vile, alisisitiza dhima ya kuwa tayari kuthubutu&nbsp; na kushindwa, akieleza kwamba &quot;si suala tu la kufanya kazi kwa bidii ili kupata muundo ulio kamili palepale mwanzoni, bali ni suala la kuunda modeli zilizo nyepesi kurekebishwa, kupimwa ili kuona ufanisi wake na hasa katika kubadilishika kwake kwa haraka ili kupata maoni, kuongeza ubora, na kufanya uendane na mahitaji, lakini pia kujaribu&nbsp; kitu kipya&rdquo;.</p><br>
<p><br>
	Mkutano huo uliandaliwa na the Open Institute na Africa Media Initiative, na kupata ufadhili wa Twaweza na makundi mengine. Twaweza inafanya majadiliano na makundi haya kuhusu namna gani demokrasia inaweza kuletwa kwenye data na kuwawezesha wananchi kuzitumia ili kuleta mabadiliko . Vile vile Twaweza imemkaribisha&nbsp; rafiki mmoja wa kutoka <a href="http://code4kenya.org/">Code4Kenya</a> katika ofisi zake za Nairobi.</p><br>
<p><br>
	Majadiliano katika mkutano huo yalirushwa na washiriki kadhaa kwa njia ya twita na, mmoja wao akiwa <a href="http://www.alkags.me/?p=576">Al Kags blog</a> ambaye alichapisha baadhi ya mijadala kwa kina zaidi kidogo kuhusu siku za mwanzo za Mkutano huo. Ripoti ya Mkutano huo itachapishwa hapa (kwa Kiingereza) siku chache zijazo.</p><br>
]]></description>
							<pubDate>Wed, 14 Nov 2012 08:58:00 +0000</pubDate>
				
				</item>
	</channel>
</rss>