Wananchi Wazungumza kuhusu Matokeo ya Kidato cha Nne
14 May 2013
hot
|
Matangazo

Wazazi wana ufahamu kuhusu mwendelezo wa kuanguka kwa ubora wa elimu ya sekondari, na kwa kiasi kikubwa wanatupa lawama kwa serikali na walimu kwa kuanguka huko. Wazazi wanaitaka serikali kuongeza idadi ya walimu waliofuzu na wenye sifa stahiki na wanaolipwa vizuri iliwasaidie kuboresha elimu nchini Tanzania.
Matokeo haya yamechapishwa katika muhtasari wa Twaweza unaoitwa Matokeo ya Mtihani wa Kidato
cha Nne: Wananchi wazungumzia mgogoro wa kujifunza Tanzania. Muhtasari huo umeandaliwa kutokana na takwimu zilizokusanywa kupitia utafiti wa Sauti za Wananchi, ambao ni utafiti wa njia ya simu za mkononi wenye sura ya uwakilishi wa kaya kitaifa kote Tanzania Bara. Wahojiwa waliombwa kueleza maoni yao kuhusu elimu, na kubaini changamoto na njia za kuongeza ubora. Takwimu zilizotumika kwenye Muhtasari huu zilikusanywa kati ya tarehe 18 Machi hadi 3 Aprili, 2013 kabla ya tangazo la serikali la kurekebisha matokeo ya Kidato Cha Nne ya mwaka 2012.
Miongoni mwa waliohojiwa, asilimia 68 ya wananchi walikuwa na taarifa kwamba matokeo ya Mitihani ya Kidato cha Nne ya 2012 yalikuwa yamechapishwa. Idadi kubwa ya wahojiwa walionesha kutambua kuanguka kwa ubora wa elimu ya sekondari katika miaka kumi iliyopita, ambapo wananchi asilimia 83 walionesha kwamba elimu ilikuwa imeporomoka. Idadi hiyo inaendana na takwimu rasmi zikiwamo zile za Wizara ya Elimu zinazojulikana kama Basic Education Statistics in Tanzania (BEST).
Endelea kusoma: elimu
pakua nyaraka
- Sauti za Wananchi, Matokeo ya mtihani wa Kidato Cha 4 | Muhtasari |
1.34 MB
- Wazazi wazungumzia matokeo ya Kidato cha 4 | Taarifa kwa Umma |
287.78 KB
- Sauti za Wananchi, Matokeo ya mtihani wa Kidato Cha 4 | Muhtasari |
1.22 MB
- Wazazi wazungumzia matokeo ya Kidato cha 4 | Taarifa kwa Umma |
291.2 KB
- Tathmini ya kiwango cha kujifunza ya Darasa la 2 | Picha kwa Waandishi |
80.69 KB
- Mwonekano wa mwenendo wa ubora wa elimu |
39.15 KB
- Ushiriki wa Wazazi | Picha kwa Waandishi |
54.71 KB
- Matokeo ya Kidata cha 4 | Powerpoint |
495.94 KB
Tafsiri
unaweza pia kupenda...
- Tukiwathamini walimu, lengo la elimu bora litatimia (13 Nov 2018)
- Je, watoto wetu wanajifunza? Tathmini ya sita ya Uwezo Tanzania (10 Apr 2017)
- JiElimishe | Uhusiano kati ya matokeo ya kujifunza na utapiamlo (22 Dec 2016)
- Hali Halisi (29 Nov 2016)
- Hali Halisi: Maoni ya wananchi juu ya elimu bila malipo ya ada. (24 Nov 2016)
- Je, watoto wetu wanajifunza? (31 Aug 2016)
- Ufunguo wa maisha? (16 Jul 2016)