Machoni mwa umma: Maoni ya wananchi juu ya upatikanaji wa taarifa
15 Jun 2015
hot
| Machapisho

Asilimia 84 ya wananchi wanaunga mkono kifungu cha sheria ya upatikanaji wa habari. Wananchi nane kati ya kumi wanaamini taarifa za mamlaka za umma zinapaswa kupatikana kwa wananchi wa kawaida (77%). Wengi wanaamini upatikanaji wa taarifa utasaidia kupunguza ama kuzuia rushwa na vitendo vingine viovu vinavyofanywa na viongozi wa umma (80%).
Haya ni matokeo ya utafiti uliofanywa na Twaweza wenye jina, Jicho la Umma: Maoni ya wananchi kuhusu upatikanaji wa habari. Taarifa za utafiti huu zimekusanywa na Sauti za Wananchi, utafiti wa kwanza barani Afrika unaofanywa kwa njia ya simu za mkononi. Utafiti huu una uwakilishi wa nchi nzima. Matokeo ya utafiti huu yamejikita kwenye taarifa zilizokusanywa kutoka kwa wananchi 1,330 wa Tanzania Bara (Zanzibar haikushiriki katika utafiti) kati ya mwezi Machi na Aprili 2015.
Wananchi wanaunga mkono uwepo wa kifungu katika sheria ya upatikanaji wa habari ambacho kitatoa adhabu kwa viongozi wasiozingatia sheria. Aslimia 47 wameonyesha kifungu hicho ni cha muhimu kwenye sheria hiyo. Mwananchi mmoja kati ya watano (21%) anataka sheria hii izilazimishe mamlaka za umma kutoa taarifa. Pamoja na hayo, washiriki wametaka watoa habari walindwe (18%).
Endelea kusoma:
Authors: Angela Ambroz
pakua nyaraka
- Machoni mwa umma | Muhtasari |
991.9 KB
- Watanzania wengi wanaunga mkono sheria ya upatikanaji wa habari | Taarifa kwa Vyombo vya Habari |
290.97 KB
- In the public eye | Muhtasari |
999.7 KB
- Most Tanzanians support an Access to Information law | Taarifa kwa Vyombo vya Habari |
302.19 KB
Tafsiri
unaweza pia kupenda...
- Matarajio lukuki: Maoni ya wananchi kuhusu sekta ya gesi (31 Aug 2015)
- Ufunguo wa maisha | Maoni ya wananchi juu ya umuhimu wa shule Muhtasari huu (16 Jul 2015)
- Usalama Wetu? Maoni ya wananchi juu ya usalama na haki (28 Apr 2015)
- Kuelekea Kura ya Maoni: Maoni ya Watanzania kuhusu Katiba Inayopendekezwa (1 Apr 2015)
- Walezi wa uwajibikaji: Ufahamu na maoni ya wananchi kuhusu taasisi za usimamizi (24 Feb 2015)
- Tanzania ifikapo mwaka 2025: Je, Watanzania wana matarajio gani na maisha yao ya baadaye? (4 Dec 2014)
- Kulinda haki za kila mtu: Maoni ya wananchi juu ya ulemavu (4 Nov 2014)