Je, Tuko Salama?
3 Mar 2014
hot
| Machapisho

Karibu nusu (46%) ya Watanzania wote wamearifu kuwa wameshawahi kushuhudia vurugu katika jamii katika kipindi cha miezi sita iliyopita, ikilinganishwa na idadi ya mtu 1 kati ya 5 (20%) anayeripoti kuwa amewahi kuibiwa kitu na wezi. Nusu (49%) ya Watanzania wote wanaripoti kuwa hawajawahi kuibiwa kitu na watu 4 kati ya 10 (37%) hawajawahi kushuhudia vurugu/ghasia katika jamii.
Matokeo haya yametolewa na Twaweza katika muhtasari wa utafiti wenye jina la Je, Tuko Salama? Wananchi watoa taarifa kuhusu hali ya usalama wa nchi. Muhtasari huu ni kwa mujibu wa takwimu kutoka Sauti za Wananchi, utafiti kwa njia ya simu za mkononi wenye uwakilishi wa kitaifa uliofanyika kwenye kaya zote Tanzania Bara.
Wananchi wameripoti kuwa, kesi nyingi walizoshawahi kusikia zinazohusu mtu kutishiwa, kupigwa mawe au kuuawa, huwa ni makundi ya watu au watu binafsi wanaoyatenda na siyo polisi au jeshi. Kwa mfano, mwananchi 1 kati ya 5 (19%) ameshawahi kusikia habari za mtu kuuawa na kundi la watu, wakati ni wananchi 2 kati ya 50 (4%) tu walioshawahi kusikia mtu kuuawa na polisi. Hata hivyo, wananchi pia wamesema kuwa polisi mara nyingi huhusika anapokutwa mtu ametishwa, kupigwa au kupondwa mawe.
Wananchi wanapokumbana na uhalifu, wangependa kuripoti polisi, ingawa, ni nusu tu ya wananchi wote (47%) wanaofanya hivyo. Idadi ni kubwa katika maeneo ya mijini ambako watu 6 kati ya 10 (59%) waliripoti kuwa wangeweza kuripoti uhalifu polisi, ikilinganishwa na maeneo ya vijijini ambako watu 4 kati ya 10 (39%) ndiyo wangefanya hivyo. Hii inaweza kusababishwa na uwepo wa polisi kwenye maeneo ya mijini kuliko vijijini. Kitaifa, kwa mujibu wa maafisa watendaji wa vijiji na wenyekiti wa mitaa/vitongoji, jamii 6 kati ya 10 (62%) haina polisi. Maeneo ya mijini yana nafuu zaidi ambapo mitaa 4 kati ya 10 (36%) tu ndiyo yenye ukosefu wa polisi, wakati maeneo ya vijijini takriban vijiji 8 kati ya 10 (76%) waliripoti kutokuwa na maofisa wa polisi.
Endelea kusoma:
Authors: Elvis Mushi
pakua nyaraka
- Je, Tuko Salama? | Muhtasari |
802.56 KB
- Vurugu katika jamii hutokea kwa wingi zaidi kuliko wizi | Taarifa kwa Vyombo vya Habari |
284.66 KB
- Are we safe? | Muhtasari |
1.2 MB
- Violence in public is much more frequent than theft | Taarifa kwa Vyombo vya Habari |
286.49 KB
Tafsiri
unaweza pia kupenda...
- Matarajio lukuki: Maoni ya wananchi kuhusu sekta ya gesi (31 Aug 2015)
- Ufunguo wa maisha | Maoni ya wananchi juu ya umuhimu wa shule Muhtasari huu (16 Jul 2015)
- Machoni mwa umma: Maoni ya wananchi juu ya upatikanaji wa taarifa (15 Jun 2015)
- Usalama Wetu? Maoni ya wananchi juu ya usalama na haki (28 Apr 2015)
- Kuelekea Kura ya Maoni: Maoni ya Watanzania kuhusu Katiba Inayopendekezwa (1 Apr 2015)
- Walezi wa uwajibikaji: Ufahamu na maoni ya wananchi kuhusu taasisi za usimamizi (24 Feb 2015)
- Tanzania ifikapo mwaka 2025: Je, Watanzania wana matarajio gani na maisha yao ya baadaye? (4 Dec 2014)